Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Aprili 20, 2024 Local time: 09:52

Mtangazaji wa zamani VOA afariki dunia


Aleck Chemponda
Aleck Chemponda

Mmoja wa watangazaji waanzilishi wa Idhaa ya Kiswahili ya Sauti ya Amerika Dr. Aleck Che-Mponda amefariki dunia. Dr. Che-Mponda alifariki dunia Jumatatu jioni katika hospitali ya Massana jijini Daresalaam, Tanzania. Alikuwa na umri wa miaka 80.

Taarifa kutoka kwa watoto wake imesema alifariki kutokana na ugonjwa wa saratani ya mifupa.

Dr. Che-Mponda alikuwa mmoja watangazaji watatu wa kwanza wa Idhaa ya Kiswahili ya Sauti ya Amerika mwaka 1962. Baadaye alikuwa mwalimu katika chuo kikuu cha Dar es salaam kwa miaka mingi, kabla ya kuingia katika siasa katika miaka ya 2000.

XS
SM
MD
LG