Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 28, 2025 Local time: 19:03

Chama kidogo Taiwan kwenye mazungumzo ya tiketi ya pamoja ya urais na chama kikuu cha upinzani


Eric Chu, mwenyekiti wa chama kikuu cha upinzani cha Taiwan Kuomintang (KMT), Hou Yu-ih, mgombea urais wa KMT, Ma Ying-jeou, rais wa zamani wa Taiwan na Ke Wen-je, mgombea urais kutoka Taiwan People's Party (TPP) wakipiga picha kufuatia mkutano huko Taipei Novemba 15,2023. AFP.
Eric Chu, mwenyekiti wa chama kikuu cha upinzani cha Taiwan Kuomintang (KMT), Hou Yu-ih, mgombea urais wa KMT, Ma Ying-jeou, rais wa zamani wa Taiwan na Ke Wen-je, mgombea urais kutoka Taiwan People's Party (TPP) wakipiga picha kufuatia mkutano huko Taipei Novemba 15,2023. AFP.

Kiongozi wa chama kidogo cha kisiasa cha Taiwan ambaye amekuwa katika mazungumzo na chama kikuu cha upinzani kwa tiketi ya pamoja ya urais hakuonyesha dalili zozote  za kusalimu amri siku ya Jumapili katika mzozo uliozuka kuhusu nani agombee urais na nani awanie makamu wa rais

Kiongozi wa chama kidogo cha kisiasa cha Taiwan ambaye amekuwa katika mazungumzo na chama kikuu cha upinzani kwa tiketi ya pamoja ya urais hakuonyesha dalili zozote za kusalimu amri siku ya Jumapili katika mzozo uliozuka kuhusu nani agombee urais na nani awanie makamu wa rais.

Suala la China, ambayo inaiona Taiwan kama eneo lake, linagubika uchaguzi wa Januari 13 wa wabunge na urais. China imeongeza shinikizo la kijeshi na kisiasa, ikiwa ni pamoja na mazoezi ya kivita ya hali ya juu, kushinikiza kisiwa hicho kukubali madai ya kujitawala ambayo Taiwan inakataa.

Baada ya majuma kadhaa ya mazungumzo makali sana juu ya kujiunga kwenye uchaguzi wa rais, Kuomintang (KMT) na chama kidogo zaidi cha Taiwan People's Party (TPP) walikubaliana Jumatano kuangalia jumla ya kura za maoni ili kuamua mgombea wa chama gani atasimama kugombea kama rais na nani kama makamu wake.

Forum

XS
SM
MD
LG