Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 28, 2025 Local time: 16:19

Chama cha SNP cha Scotland chapigia debe Uhuru kwenye uchaguzi mkuu


Chama cha Kitaifa cha Scotland (SNP) kitapambana katika uchaguzi mkuu ujao nchini Uingereza kwa ujumbe mkuu wa kupigania uhuru katika kampeni zake, Waziri kiongozi Humza Yousaf amesema Jumamosi

Akihutubia mkutano wa chama tawala cha Scotland katika mji wa Dundee, Yousaf aliapa kuwa ataanzisha mazungumzo mapya na serikali ya ufalme wa Uingereza kuhusu uhuru ikiwa chama chake cha SNP kitashinda viti vingi zaidi vya nchini humo katika uchaguzi unaotarajiwa kufanyika mwakani.

“Niseme wazi, SNP ikishinda uchaguzi huu, wananchi watakuwa wamezungumza,” alisema.

"Tutatafuta mazungumzo na serikali ya ufalme wa Uingereza kuhusu jinsi tunavyo changia katika demokrasia kwa Scotland kuwa taifa huru.”

Matamshi ya Yousaf yanakuja huku uungwaji mkono wa umma ukipungua kwa chama cha SNP baada ya kukamatwa kwa kiongozi wake wa zamani na waziri wa kwanza Nicola Sturgeon, kiongozi mkuu wa harakati za kudai uhuru katika miaka ya hivi karibuni.

Mkutano wa Dundee ni mkutano wa kwanza wa ana kwa ana tangu Yousaf, 38, achukue nafasi yake mwezi Machi, na chama kilianza kuona mteremko mkubwa katika umaarufu wake.

Forum

XS
SM
MD
LG