Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Aprili 25, 2025 Local time: 08:59

Canada kuomba msaada wa Mfalme Charles wa kulinda utaifa wake.


Waziri Mkuu wa Canada Justin Trudeau akiwasili kwenye uwanja wa ndege wa jeshi wa Andrews, Maryland, July 8, 2024, ili kuhudhuria mkutano wa mjini Washington.
Waziri Mkuu wa Canada Justin Trudeau akiwasili kwenye uwanja wa ndege wa jeshi wa Andrews, Maryland, July 8, 2024, ili kuhudhuria mkutano wa mjini Washington.

Waziri Mkuu wa Canada Justin Trudeau Jumapili amesema kwamba atazungumza na Mfalme Charles wa Uingereza hukusu kulindwa kwa utaifa wa Canada baada ya tishio la mara kwa mara kutoka kwa rais wa Marekani Donald Trump kwamba itafanywa kuwa jimbo la 51 la Marekani.

Matamshi ya Trump yamewaghadhabisha wengi nchini Canada, wakati maafisa wakipinga vikali uwezekano wa mashauriano ya aina yoyote ile ya kuifanya Canada kuwa sehemu ya Marekani.

Wakati akikutana na Mfalme Charles ambaye ndiye kiongozi wa taifa la Canada Jumanne, Trudeau alisema kuwa wangezungumzia maswala muhimu ya Canada pamoja na watu wake.

Tangu kuingia madarakani mwaka huu, Trump amekuwa akiitaja Canada mara kwa mara kama jimbo la 51 la Marekani na hata kumuita Waziri Mkuu Trudeau, Gavana.

Trump ameamuru ushuru uwekwe dhidi ya mshirika mkuu wa kibiashara wa Marekani, na vinapangwa kuanza Jumanne, wakati akisema huenda hilo linaweza kuepukika kama Canada itakuwa sehemu ya Marekani.

Mwezi uliopita, Trudeau alionya kuwa tishio la Trump la mara kwa mara kuhusu kuichukua Canada ili kufikia rasilimali zake asili “ni suala la kweli.”Baadhi ya raia wa Canada wanasema kwamba hawaelewi kwanini Mfalme Charles hajazungumza kuitetea Canada.

Forum

XS
SM
MD
LG