Cameroon kwa mara ya kwanza imewaruhusu watafiti kutoka shirika la kimataifa la haki za binadamu Amnesty International kuingia nchini humo kwa ziara rasmi.
Watafiti hao waliondoka Cameroon leo baada ya siku 10 za mikutano na maafisa kujadli wasi wasi wao juu ya haki za binadamu.
Godfrey Byaruhanga wa Amnesty International aliiambia sauti ya Amerika kuwa alifurahishwa kupata fursa hiyo. Alisema maafisa walionyesha nia ya kulinda haki za binadamu lakini labda hawana rasilimali na utaalam.