Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Aprili 18, 2024 Local time: 22:32

Burkina Faso yazindua kiwanda chake cha kwanza cha kutengeneza dawa za bei nafuu


Waziri mkuu wa Burkina Faso Albert Ouedraogo akizungumza kwenye mkutano wa kwanza wa baraza la mawaziri la serikali mpya , Machi 7, 2022. Picha ya AFP
Waziri mkuu wa Burkina Faso Albert Ouedraogo akizungumza kwenye mkutano wa kwanza wa baraza la mawaziri la serikali mpya , Machi 7, 2022. Picha ya AFP

Waziri mkuu wa Burkina Faso Albert Ouedraogo Jumanne alitembelea kiwanda cha kwanza cha kutengeneza dawa cha nchi hiyo, ambacho kitatengeneza dawa zenye gharama nafuu kama vile paracetamol.

Kiwanda hicho ambacho kilijengwa na ufadhili wa kibinafsi kwenye eneo la hekta 1.5 huko Komsilga, katika kitongoji cha mji mkuu, kitahakikisha dawa zinazotumiwa na watu wengi zinapatikana, maafisa wamesema.

Kitaanza kutengeneza katika miezi michache ijayo dawa kama vile paracetamol na dawa ya kurejesha maji mwilini kwa ajili ya kutibu ugonjwa wa kuhara, mkurugenzi mkuu Armel Coefe amesema.

“Uwezo wetu wa uzalishaji kwa sasa unakidhi mahitaji ya ndani na utasuluhisha tatizo la upungufu mkubwa wa uzambazaji,” Coefe amesema.

Waziri mkuu Ouedraogo amesema kiwanda hicho ni cha “muhimu kwa sababu kitasaidia kuwapatishia raia dawa za bei nafuu.”

XS
SM
MD
LG