Mswaada huo unataka kubatilisha uamuzi wa mahakama ya juu ambao uliruhusu uhalali wa baadhi ya ndoa zilizofanyika nje ya nchi.
Sheria hiyo ilipitishwa na bunge bila upinzani wowote.
“Muungano wa familia ni kati ya mwanaume na mwanamke na hilo lazima liheshimiwe,” Mzee Filipe, mbunge wa chama tawala cha SWAPO aliliambia bunge.
Sheria hiyo inafafanua upya “ndoa” kama muungano “kati ya watu wa jinsia tofauti”.
Inasisitiza kuwa ndoa za jinsia moja zilizofanyika nje ya nchi hazitambuliwi nchini Namibia.
Forum