Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Januari 18, 2025 Local time: 13:38

Bunge la Algeria lapitisha sheria kali inayominya uhuru wa vyombo vya habari


Gazeti la Algeria "Liberte" linalochapisha habari katika lugha ya Kifaransa, laonekana kwenye duka katika mji mkuu wa Algeria, Aprili 14, 2022.
Gazeti la Algeria "Liberte" linalochapisha habari katika lugha ya Kifaransa, laonekana kwenye duka katika mji mkuu wa Algeria, Aprili 14, 2022.

Bunge la Algeria Alhamisi lilipitisha sheria inayominya zaidi uhuru wa vyombo vya habari katika nchi hiyo ya Afrika Kaskazini kwa kuweka sheria kali za umiliki wa vyombo vya habari na kuwazuia waandishi wa habari kulinda vyanzo vyao.

Sheria hiyo inapiga marufuku vyombo vya habari vya ndani kupokea ufadhili au msaada wa vifaa wa moja kwa moja au usio wa moja kwa moja kutoka nje, chini ya tishio la kufunguliwa mashtaka ya uhalifu ikiwemo faini ya hadi dola 15,000.

Inakubali kuwa siri ya kitaalamu ni haki, lakini inaruhusu mahakama kuwalamizisha waandishi wa habari kufichua vyanzo vyao.

Inapiga pia marufuku kwa watu wenye uraia pacha kumiliki vyombo vyote vya habari au sehemu ya vyombo hivyo, na waandishi wa habari wanaofanyia kazi vyombo vya habari vya kigeni bila kibali, wanaweza kutozwa faini ya dola 7,600.

XS
SM
MD
LG