Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Machi 20, 2023 Local time: 20:06

Bomu lajeruhi watu 17 ndani ya soko mashariki mwa DRC


Ramani ya Beni, DRC

Watu 17 walijeruhiwa Jumatano wakati bomu lilipolipuka ndani ya soko mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, maafisa wamesema, huku eneo hilo likiendelea kukumbwa na ukosefu wa usalama.

Bomu hilo lililipuka ndani ya soko la Macampagne katika mji wa Beni, ambako watu 17 walijeruhiwa na kupelekwa kwenye vituo vya matibabu, amesema Tharcisse Katembo, mkuu wa wilaya huko Beni.

Mwandishi wa AFP aliona watu wanane waliojeruhiwa, wakiwemo wasichana watatu, wakihudumiwa kwenye hospitali.

Waathirika walipata majeraha kwenye miguu, mikono na kichwani, mwandishi huyo amesema.

“Kijana mmoja aliacha mfuko wa plastiki wa rangi ya kijani kibichi, akiahidi kurejea kuuchukua. Dakika tatu baadaye, mfuko huo ulilipuka na kuwajeruhi watu na mimi nikiwemo na wateja waliokuja kusaga mihogo,” Dany Siauswa, meneja wa kiwanda hicho cha kusaga, ameiambia AFP.

Facebook Forum

XS
SM
MD
LG