Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Februari 15, 2025 Local time: 12:07

Bolsonaro aidhinisha kuanza mchakato wa mpito na wawakilishi wa Rais mteule Lula da Silva


Rais mteule wa Brazil Luiz Lula da Silva akiwa na Waziri wa zamani wa Mazingira Marina Silva nawakikumbatiana wakati wa mkutano na waandishi wa habari mjini Sao Paulo, Brazili Septemba 12, 2022. REUTERS
Rais mteule wa Brazil Luiz Lula da Silva akiwa na Waziri wa zamani wa Mazingira Marina Silva nawakikumbatiana wakati wa mkutano na waandishi wa habari mjini Sao Paulo, Brazili Septemba 12, 2022. REUTERS

Rais wa Brazil Jair Bolsonaro siku ya Jumanne hakukubali kutangaza kushindwa katika matamshi yake ya kwanza hadharani tangu kushindwa katika uchaguzi wa Jumapili.

Rais huyo alisema maandamano ya wafuasi wake yalikuwa matunda ya "ghadhabu na hisia ya ukosefu wa haki" kuhusu kura hiyo.

Hata hivyo, hakusema kuwa anapinga matokeo ya uchaguzi huo na kuidhinisha mkuu wake wa wafanyakazi wa Ikulu, Ciro Nogueira, kuanza mchakato wa mpito na wawakilishi wa Rais mteule wa mrengo wa kushoto Luiz Inacio Lula da Silva.

Ilimchukua Bolsonaro, mzalendo wa mrengo wa kulia, zaidi ya saa 44 kutoa maoni yake baada ya uchaguzi kuamuliwa na mamlaka ya uchaguzi, huku ucheleweshaji huo ukizua hofu kwamba angetaka kutilia shaka matokeo hayo waliopishana kwa kura chache.

Katika ukimya wake wafuasi wake walifunga barabara kuu kupinga kushindwa kwake, huku wengine wakitaka mapinduzi ya kijeshi kumzuia rais wa zamani Lula kurejea madarakani.

Vizuizi hivyo vya barabara kuu vimetatiza usambazaji wa mafuta, usambazaji wa maduka makubwa na usafirishaji wa nafaka kwenye bandari kuu, kulingana na vikundi vya sekta hiyo.

XS
SM
MD
LG