Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Januari 24, 2025 Local time: 02:24

Blinken akutana na Rais wa Palestina Mahmoud Abbas


PICHA YA MAKTABA: Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Antony Blinken (Kushoto) na rais wa mamlaka ya Palestina, Mahmoud Abbas
PICHA YA MAKTABA: Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Antony Blinken (Kushoto) na rais wa mamlaka ya Palestina, Mahmoud Abbas

Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Antony Blinken alijadili mageuzi ya kiutawala na Rais wa Palestina Mahmoud Abbas wakati wa mkutano wao leo Jumatano katika Ukingo wa Magharibi, pamoja na juhudi za kuimarisha misaada ya kibinadamu kwa watu wa Ukanda wa Gaza.

Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani Matthew Miller alisema katika taarifa yake kwamba Blinken "kwa mara nyingine alisisitiza kwamba Marekani inaunga mkono hatua zinazoonekana kuelekea kuundwa kwa taifa la Palestina pamoja na Taifa la Israeli, na wote wanaishi kwa amani na usalama."

Blinken pia aliitaka Israeli kuhamishia mapato yote ya kodi ya Wapalestina inazokusanya kwa mamlaka ya Palestina kwa mujibu wa makubaliano yaliyopo.

Mamlaka ya Palestina inatawala sehemu ya Ukingo wa Magharibi, huku kundi la wanamgambo wa Hamas likidhibiti Ukanda wa Gaza ambako Israeli inapigania kulitokomeza kundi hilo. Marekani imetazamia mpango madhubuti wa baada ya vita, ambao utaiweka Gaza chini ya utawala unaoongozwa na Wapalestina bila jukumu lolote kwa Hamas.

Lakini wachambuzi wengine wana mashaka na matarajio hayo.

Blinken amesisitiza uwezekano wa Israel kukubalika na majirani wake wa Kiarabu kwa kutafuta njia kuelekea kuanzisha taifa la Palestina kama njia ya kutatua mzozo huo.

Netanyahu amekataa katakata suluhisho la mataifa mawili.

Forum

XS
SM
MD
LG