Rais Joe Biden Jumatatu alitoa amri ya kuzuia kampuni ya madini ya cryptocurrency inayoungwa mkono na China kumiliki ardhi karibu eneo la kituo cha nyuklia huko Wyoming.
Amri hiyo inalazimisha mgawanyiko wa mali inayoendeshwa kama kituo cha madini ya crypto karibu na Kambi ya Jeshi la Anga la Francis E. Warren. Pia inalazimisha kuondolewa kwa vifaa fulani vinavyomilikiwa na MineOne Partners Ltd, kampuni ambayo kwa sehemu inamilikiwa na serikali ya China.
Haya yanajiri wakati Marekani ikitarajiwa Jumanne kutoa ushuru mkubwa kwa magari ya umeme, vifaa vya nishati ya jua na vifaa vya matibabu vilivyoagizwa kutoka China, kulingana na afisa wa Marekani na mtu mwingine anayefahamu mpango huo.
Amri hiyo ya mgawanyo ilitolewa kwa ushirikiano na Kamati ya Marekani ya Uwekezaji wa Nje nchini Marekani, haifahamiki sana lakini ina nguvu iliyopewa jukumu la kuchunguza mikataba ya kampuni inayotia wasiwasi wa usalama wa kitaifa ambapo ina nguvu ya kuilazimisha kampuni hiyo kufanya mabadiliko.
Forum