Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Mei 18, 2025 Local time: 22:23

Biden ametoa amri ya kuzuia kampuni ya madini kumiliki ardhi huko Wyoming


Rais Biden amezuia kampuni ya madini kumiliki ardhi karibu na kituo cha jeshi la anga- F.E. Warren Air Force Base. May 24, 2018. Cheyenne, Wyoming.
Rais Biden amezuia kampuni ya madini kumiliki ardhi karibu na kituo cha jeshi la anga- F.E. Warren Air Force Base. May 24, 2018. Cheyenne, Wyoming.

Pia inalazimisha kuondolewa kwa vifaa vinavyomilikiwa na MineOne Partners ambayo kwa sehemu inamilikiwa na serikali ya China.

Rais Joe Biden Jumatatu alitoa amri ya kuzuia kampuni ya madini ya cryptocurrency inayoungwa mkono na China kumiliki ardhi karibu eneo la kituo cha nyuklia huko Wyoming.

Amri hiyo inalazimisha mgawanyiko wa mali inayoendeshwa kama kituo cha madini ya crypto karibu na Kambi ya Jeshi la Anga la Francis E. Warren. Pia inalazimisha kuondolewa kwa vifaa fulani vinavyomilikiwa na MineOne Partners Ltd, kampuni ambayo kwa sehemu inamilikiwa na serikali ya China.

Haya yanajiri wakati Marekani ikitarajiwa Jumanne kutoa ushuru mkubwa kwa magari ya umeme, vifaa vya nishati ya jua na vifaa vya matibabu vilivyoagizwa kutoka China, kulingana na afisa wa Marekani na mtu mwingine anayefahamu mpango huo.

Amri hiyo ya mgawanyo ilitolewa kwa ushirikiano na Kamati ya Marekani ya Uwekezaji wa Nje nchini Marekani, haifahamiki sana lakini ina nguvu iliyopewa jukumu la kuchunguza mikataba ya kampuni inayotia wasiwasi wa usalama wa kitaifa ambapo ina nguvu ya kuilazimisha kampuni hiyo kufanya mabadiliko.

Forum

XS
SM
MD
LG