Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Aprili 20, 2025 Local time: 09:52

Biden amekutana na viongozi wa Korea kusini na Japan kujadili Korea kaskazini


Kiongozi wa Korea kaskazini Kim Jong Un akifuatiliaa majaribio ya makombora ya masafa marefu March 16, 2023
Kiongozi wa Korea kaskazini Kim Jong Un akifuatiliaa majaribio ya makombora ya masafa marefu March 16, 2023

Rais wa Marekani Joe Biden, amefanya kikao na washirika wawili wakuu wa huko Asia, waziri mkuu wa Japan Fumio Kashida na rais wa Korea kusini Yoon Suk Yeol, ikiwa ni ishara ya uhusiano mwema kati ya Marekani na mataifa hayo mawili ya barani Asia.

Kikao hicho pembeni ya mkutano wa viongozi wa nchi saba zenye uchumi mkubwa duniani, mjini Hiroshima, Japan, viongozi hao wamezungumzia tishio la silaha za nyuklia la Korea kaskazini na ushawishi wa China unaoongezeka.

Taarifa ya White House imesema kwamba viongozi hao wamejadiliana namna ya kuimarisha uhusiano wao wa kiusalama kutokana na tichio la Korea Kaskazini, pamoja na kiuchumi.

Viongozi hao vile vile wamejadiliana kuhusu changamoto za kiuchumi wanazokabiliana nazo kutokana na hatua kali za kibiashara zinazowekwa na jamhuri ya watu wa China kwa maslahi yake.

XS
SM
MD
LG