Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumanne, Aprili 22, 2025 Local time: 12:42

Biden ahudhuria mkutano wa G-20, Indonesia


Rais wa Marekani Joe Biden akizingumza na rais wa Indonesia, Joko Widodo. REUTERS Jumatatu Novemba 14, 2022
Rais wa Marekani Joe Biden akizingumza na rais wa Indonesia, Joko Widodo. REUTERS Jumatatu Novemba 14, 2022

Rais wa Marekani Joe Biden ameungana na viongozi wengine wa dunia, katika kisiwa cha mapumziko cha Bali nchini Indonesia .

Biden anahudhuria mkutano wa G-20, ambapo rais wa taifa hilo Joko Widodo ni mwenyeji wa mkutano huo. Katika mazungumo yake na Widodo pembeni ya mkutano huo, Biden amemtania na kusema kwamba “ sidhani nataka kurejea kwetu tena.

” Kikao cha viongozi hao kinaonkeana kupunguza taharuki ya kidiplomasia kati ya Washington na Jarkata, kabla ya mkutano wa G-20 unaozileta pamoja nchi wanachama 20 wenye nguvu ulimwenguni.

Hilo linafanyika wakati macho yakiwa yameelekezwa kwenye vita vya Ukraine, kukiwa na shinikizo la kuitenga Russia kutoka mataifa ya magharibi.

Rais wa Russia Vladimir Putin hatahudhuria mkutano huo, na wala haijabainika iwapo atashiriki kwa njia ya mtandao. Hata hivyo mwenzake wa Ukraine Volodmyrr Zelenskyy atahurudhuria kwa njia ya mtandao. licha ya kuwa Ukraine siyo mwanachama wa G-20.

XS
SM
MD
LG