Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 15:02

Belarus yajibu vikwazo vya Marekani


Rais wa Belarus Alexander Lukashenko
Rais wa Belarus Alexander Lukashenko

Serekali ya kiongozi wa Belarus Alexander Lukashenko imelipiza kisasi kwa vikwazo vya hivi karibuni vya Marekani, kwa kuiomba Washington kupunguza wafanyakazi wake kwenye ubalozi wake mjini Minsk hadi watu watano ifikapo tarehe mosi Septemba.

Msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya Belarus, Anatol Glaz, amesema katika mahojiano ambayo yamewekwa kwenye tovuti ya wizara hiyo Agosti 11, kwamba Minsk pia imebatilisha idhini yake ya kuteuliwa kwa Julie Fisher kama balozi wa Marekani nchini Belarus.

“Kwa kuzingatia kwamba Belarus haina tena uaminifu kwa utawala wa sasa wa Marekani, tunasimamisha ushirikiano katika miradi yote mipya, misaada na mipango inayoratibiwa na serekali ya Marekani hadi uaminifu huo utakaporejea,” Glaz amesema, akiongeza kuwa Minsk itakua na haki ya kutangaza hatua za ziada katika siku zijazo.

XS
SM
MD
LG