Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 28, 2025 Local time: 16:33

Baraza la Wawakilishi Marekani lapitisha ajenda ya Trump kupunguza kodi


Spika wa Baraza la Wawakilishi Mike Johnson akiwa katika Bunge la Marekani, Washington, Feb. 25, 2025.
Spika wa Baraza la Wawakilishi Mike Johnson akiwa katika Bunge la Marekani, Washington, Feb. 25, 2025.

Spika wa baraza la wawakilishi la Marekani, Mike Johnson alipata kura za kutosha 217-215,  ili kupitisha azimio la bajeti Jumanne usiku.

Hatua hii ni kuendeleza juhudi za chama cha Republican za kuongeza muda wa ziada wa kulipa kodi na kupunguza matumizi ambayo Wademokrat wameyaita yasiyo na msingi.

Johnson na viongozi wa Warepublikan kwenye Baraza la Wawakilishi wamesema katika taarifa kuwa lengo lao ni mswada wa kulinda mpaka, kupunguza kodi kwa familia na wazalishaji wa ajira, kurejesha utawala wa nishati wa Marekani.

Pia ni kuimarisha msimamo wa Marekani ulimwenguni, huku serikali ikifanyakazi kwa ufanisi zaidi.

Rais wa Marekani Donald Trump akizungumza katika mkutano wa Baraza la Mawaziri huko White House mjini Washington, DC, Februari 26, 2025.
Rais wa Marekani Donald Trump akizungumza katika mkutano wa Baraza la Mawaziri huko White House mjini Washington, DC, Februari 26, 2025.

Spika Johnson alieleza kuwa: “Tuna kazi ngumu sana mbele yetu, lakini tutawasilisha ajenda ya Marekani Kwanza. Tutawasilisha yote, sio baadhi ya sehemu zake tu. Hii ni hatua ya kwanza katika mchakato huo.”

Rais Donald Trump ametoa wito kwa wabunge kupitisha mswada anaouita “mkubwa na mzuri” ambao utakuwa sehemu muhimu ya kutekeleza ajenda zake katika sera ya mambo ya ndani.

Forum

XS
SM
MD
LG