Katika taarifa iliyokubaliwa kwa maafikiano, baraza hilo lenye wanachama 15 limesema marufuku kwa wanawake na wasichana kusoma kwenye shule za sekondari na vyuo vikuu nchini Afghanistan “inawakilisha mmomonyoko unaoongezeka wa kuheshimu haki za binadamu na misingi ya uhuru.”
Marufuku kwa wanawake kusoma kwenye vyuo vikuu ilitangazwa wiki iliyopita, wakati Baraza la usalama likikutana mjini New York kujadili hali ya Afghanistan.
Wasichana walipigwa marufuku kusoma kwenye shule za sekondari tangu mwezi Machi.