Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Mei 02, 2024 Local time: 11:19

Azory Gwanda: Serikali ya Tanzania yatakiwa kutoa maelezo kuhusu "kifo" chake


Azory Gwanda mwandishi habari wa gazeti la Mwananchi
Azory Gwanda mwandishi habari wa gazeti la Mwananchi

Kamati ya kulinda haki za wanahabari CPJ, imetoa wito kwa serikali ya Tanzania kutoa maelezo ya kina kuhusu hatima ya mwandishi wa habari wa kujitegemea Azory Gwanda, baada ya waziri wa Mambo ya nje wa taifa hilo Palamagamba Kabudi kukiri kwamba Gwanda alikufa.

Katika mahojiano na shirika la habari la BBC kipindi cha Focus on Africa siku ya Jumatano, Kabudi alisema kuwa Gwanda alitoweka na kufa kwenye eneo Rufiji, mashariki mwa Tanzania.

Aliongeza kuwa tangu kisa hicho kutokea serikali imeweza kudhibiti hali na hasa kwenye eneo la tukio.

Gwanda alitoweka Novemba 21, 2017 baada ya kufuatilia habari kuhusu mauaji ya kutatanisha pamoja na kutoweka kwa watu miongoni mwa jamii yake.

Kwa mujibu wa kamati ya CPJ, hadi sasa serikali haijatoa maelezo kufuatia ahadi yake ya kuchunguza kisa hicho.

Kabudi aliongeza kwamba serikali ya Tanzania haijafurahishwa na kupotea kwa watu pamoja na mauaji ya Rufiji ambayo anasema yametokea kwa maafisa wa polisi pamoja na viongozi wa kisiasa na kwamba wanafanya kila wawezalo kuhakikisha usalama wa raia pamoja na waandishi wa habari.

-Imetayarishwa na Mwandishi wa VOA, Harrison Kamau.

XS
SM
MD
LG