Inaelezwa lilipangwa kutekelezwa na vijana watatu ambao wanadaiwa kuunga mkono kundi la Islamic State.
Mkuu wa idara ya upelelezi ya Austria aliwaambia waandishi wa habari kwamba washukiwa hao, wenye umri wa miaka 14, 17 na 20, walikamatwa saa moja kabla ya kuanza kwa gwaride la Jumamosi la Pride, ambalo lilihudhuriwa na karibu watu 300,000, radio ya taifa ya ORF iliripoti.
Omar Haijawi-Pirchner kutoka idara ya Usalama wa taifa na ujasusi amesema hakukuwa na hatari kwa washiriki wa gwaride wakati wote.
Kansela wa Austria, Karl Nehammer alitoa shukrani zake kwa wapelelezi kwa kuzuia shambulio hilo Vienna.
Kupitia ujumbe wa Twittr alisema “hii inaonyesha kwa mara nyingine hatupaswi kamwe kujitoa katika vita dhidi ya watu wenye itikadi kali."
Forum