Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatano, Januari 15, 2025 Local time: 08:51

Australia kuendesha zoezi la kuwasaka wasafirishaji haramu wa binadamu


Kuongezeka kwa biashara ya usafirishaji haramu wa binadamu Australia.
Kuongezeka kwa biashara ya usafirishaji haramu wa binadamu Australia.

Australia inasema itapambana na ongezeko la visa feki ambazo zimeruhusu usafirishaji haramu wa binadamu kutodhibitiwa baada ya uchunguzi wa serikali kuonyesha kuwa “unyanyasaji wa kuchukiza” kwa wahamiaji wa muda, ikiwemo kuwatumia kingono na usafirishaji haramu wa binadamu.

Serikali ya Australia ilisema Alhamisi kuwa chombo cha kudhibiti wahamiaji nchini kinashindwa kutekeleza wajibu wake.

Waziri wa Mambo ya Ndani Clare O”Neil aliwaambia waandishi wa habari mapungufu katika mfumo wa uhamiaji, ikiwemo upungufu wa wafanyakazi, umeruhusu magenge ya kihalifu ya kimataifa kuwasafirisha waathirika wa biashara hiyo haramu kuwaleta Australia kwa madai ya utapeli ya kutafuta hifadhi au visa za utalii ambazo inatakikana zikaguliwe na kufuatiliwa na serikali.

Magenge hayo baadae huwalazimisha waathirika hao kuingia katika ukahaba nchini Australia.

O’Neil ameiita hali hiyo “kuwa ni ulaghai wa kustaajabisha ambao umetendwa kwa watu wa Australia.”

Shirika la Kimataifa la Kazi, ILO, na wanaharakati wa haki za binadamu wanakadiria kuwa kuna watu 15,000 ambao wamewekwa katika mazingira yanayo fanana na utumwa nchini Australia.

Msichana Mromania aliyekuwa akifanyishwa ukahaba akiwa katika hifadhi huko Romania Novemba 30,2006.
Msichana Mromania aliyekuwa akifanyishwa ukahaba akiwa katika hifadhi huko Romania Novemba 30,2006.

Mbali na wanawake wanaolazimishwa katika ukahaba, wapo wanaolazimishwa kuolewa, na pia wanaofanya kazi katika viwanda, migahawa au usafishaji.

Serikali pia ilisema kuwa madai uongo ya kutafuta hifadhi yanawawezesha waombaji kubakia Australia kwa takriban muongo moja huku wakiwa na visa za muda kabla ya kesi zao kutatuliwa.

Programu mbalimbali za elimu ya kimataifa, ambayo wanafunzi wa kigeni wanakuja kusoma Australia pia imebainika kuwa ni eneo linalo saidia kuingiza wahamiaji haramu na utoaji wa visa feki.

O’Neil aliliambia Shirika la Utangazaji la Australia kuwa udanganyifu umeenea katika mfumo wa utoaji visa.

Ripoti ya mwandishi wa VOA Phil Mercer.

Forum

XS
SM
MD
LG