Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Februari 06, 2025 Local time: 16:06

Askari watatu wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa wauawa na wengine watatu wajeruhiwa


Wanajeshi wa Mali wakiwa wakati wa doria na askari wa kikosi cha Takuba karibu na mpaka wa Niger katika eneo la Dansongo, Mali Agosti 23, 2021. (REUTERS).
Wanajeshi wa Mali wakiwa wakati wa doria na askari wa kikosi cha Takuba karibu na mpaka wa Niger katika eneo la Dansongo, Mali Agosti 23, 2021. (REUTERS).

Askari watatu wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa waliuawa na wengine watatu kujeruhiwa vibaya wakati gari lao lilipogonga kilipuzi kaskazini mwa Mali siku ya Jumatatu, msemaji wa Umoja wa Mataifa alisema.

Wanamgambo wa Kiislamu, wenye uhusiano na al-Qaida na kiundi la Islamic State, wamekuwa wakiendesha uasi kaskazini mwa Mali kwa muongo mmoja uliopita.

​Askari wa kulinda amani walikuwa kwenye doria ya utafutaji na kugundua mabomu ya Ardhini katika wilaya ya kaskazini ya Tessalit, katika mkoa wa Kidal, wakati waliposhambuliwa , msemaji wa Stephane Dujarric aliwaambia waandishi wa habari.

Tunatuma salamu zetu za rambirambi kwa familia za walinda amani, kwa wenzetu katika operesheni hii na tunawatakia ahueni ya haraka wale waliojeruhiwa," Dujarric alisema.

MINUSMA -Jeshi la Umoja wa Mataifa la Kuleta Utulivu wa pande zote nchini Mali kwa sasa una wanajeshi wapatao 12,000 waliotumwa nchini humo.

XS
SM
MD
LG