Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 17:24

Al-Shabaab yaua maafisa watano wa Polisi Kenya


Maafisa wa polisi nchini Kenya wakiwa katika doria
Maafisa wa polisi nchini Kenya wakiwa katika doria

Maafisa watano wa Polisi nchini Kenya wameuwawa baada ya gari lao kushambuliwa na wanachama wa kikundi cha al-Shabaab Jumatano.

Maafisa wa serikali wamesema askari watatu wastaafu na wawili wa ngazi ya juu waliuwawa wakati wakisafiri kwenye kaunti ya Kaskazini, karibu na eneo linalopakana na Somalia.

Kikundi hicho cha al-Shabaab kilichoko Somalia kimefanya mashambulizi kadhaa nchini Kenya tangia mwaka 2011, ikilipiza kisasi kitendo cha Kenya kupeleka vikosi vyake nchini Somalia ikiwa ni hatua ya kuwaondoa al-Shabaab katika mji mkuu wa Mogadishu, ikiwa ni sehemu ya walinda amani wa Umoja wa Afrika na majeshi ya ulinzi ya Somalia.

Al-Shabab imeendelea kufanya mashambulizi nchini Somalia wakijaribu kupindua serikali na kuweka utawala wa Kiislam wenye msimamo mkali. Imefanya mashambulizi ya kutega mabomu dhidi ya serikali, jeshi na raia.

XS
SM
MD
LG