Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Februari 10, 2025 Local time: 22:02

Ajali ya ndege Kazakhstan baada ya kugonga nyuni


Mabaki ya ndege ya shirika la Azerbaijan iliyoanguka karibu na mji wa Aktau, Kazakhstan Desemba 25, 2024. REUTERS
Mabaki ya ndege ya shirika la Azerbaijan iliyoanguka karibu na mji wa Aktau, Kazakhstan Desemba 25, 2024. REUTERS

Uchunguzi wa awali unasema kwamba ndege ya shirika la ndege la Azerbaijan iliyoanguka na kusababisha vifo vya zaidi ya watu 30, ilitokana na ndege hiyo kugonga ndege mnyama.

Taarifa zinasema kwamba ndege hiyo ililazimika kubadilisha safari kuelekea Aktau kutokana na tukio la dharura kwa abiria.

Ndege ya shirika la Azerbaijan, Embraer 190 kutoka Baku kuelekea Grozny, imeanguka mapema Jumatano, karibu na uwanja wa ndege wa Aktau.

Maafisa wanasema watu 30 wamefariki na 28 kunusurika.

Ndege hiyo ilishika moto baada ya kuanguka.

Wizara ya maswala ya dharura ya Kazakhstan imesema maafisa wa uokoaji 52 walitumwa katika eneo la ajali kwa ajili ya uokoaji.

Ndege ilikuwa na abiria 62 na wafanyakazi watano.

Shirika la ndege la Azerbaijan limethibitisha tukio hilo na kuahidi taarifa zaidi baadaye. Uchunguzi unaendelea.

Forum

XS
SM
MD
LG