Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Aprili 19, 2024 Local time: 10:22

Abiy aapa kutekeleza makubaliano ya kusitisha mapigano kati ya serikali yake na waasi wa Tigray


Waziri mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed
Waziri mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed

Waziri mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed Jumanne ameapa kutekeleza kwa uaminifu makubaliano ya kusitisha mapigano kati ya serikali yake na vikosi vya Tigray, ambayo amesema ni muhimu ili kuhakikisha amani ya kudumu inapatikana.

Makubaliano hayo yaliyosainiwa tarehe 2 Novemba yaliridhia kumaliza vita vya miaka miwili ambavyo viliharibu eneo la Tigray, kuua maelfu ya watu, kuwahamisha kwenye makazi yao mamilioni ya watu na kutishia umoja wa taifa hilo la pili lenye idadi kubwa ya watu barani Afrika.

Serikali ya Abiy na wawakilishi kutoka Tigray Jumamosi walisaini makubaliano zaidi ya kutekeleza usitishaji mapigano.

“Tumepiga hatua moja mbele, tumejadiliana, tumekubaliana na kutia saini. Jambo la kufuata linalotarajiwa kutoka kwetu litakuwa kutekeleza kwa uaminifu kile tulichoahidi kufanya amani idumu,” Abiy ameliambia bunge la Ethiopia baada ya kusikiliza masuali ya wabunge.

XS
SM
MD
LG