Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Januari 13, 2025 Local time: 13:38

Abiria 11 waliotekwa nyara Kaskazini mwa Nigeria waachiliwa huru


Wanawake wa sokoni wakiandamana nje ya Ikulu ya Olowo ya Owo, kufuatia shambulio la Jumapili katika Kanisa Katoliki la St. Francis huko Owo, Nigeria, Jumanne, Juni 7, 2022.
Wanawake wa sokoni wakiandamana nje ya Ikulu ya Olowo ya Owo, kufuatia shambulio la Jumapili katika Kanisa Katoliki la St. Francis huko Owo, Nigeria, Jumanne, Juni 7, 2022.

Watu wenye silaha wamewaachilia huru abiria 11 ambao walitekwa nyara wakati wa shambulio la treni kaskazini mwa Nigeria mwishoni mwa mwezi Machi, waziri wa serikali alisema, ingawaje darzeni ya wengine wanadhaniwa bado wameshikiliwa mateka.

Gbemisola Saraki, waziri wa serikali wa uchukuzi, alisema katika taarifa Jumamosi usiku kwamba serikali ilikuwa inafanya kazi kuhakikisha abiria wote waliotekwa nyara wameachiliwa huru.

Abiria walioachiliwa huru walipelekwa katika hospitali moja mjini Abuja. Saraki hakusema jinsi gani na wapi waliachiliwa huru au ikiwa fidia ililipwa.

Magenge ya watu wenye silaha, wanaojulikana kama majambazi, walilipua njia ya reli ya Abuja-Kaduna kaskazini mwa nchi hiyo na kufyatua risasi kwenye treni ya usiku Machi 28, na kuua watu wanane.

XS
SM
MD
LG