Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 10:52

Shirika la Mafuta la serikali Libya laonya Marekani


Shirika la mafuta la serikali ya Libya limeonya mashirika ya mafuta ya Marekani kuhusu uwezekano wa kukumbana na matokeo mabaya kufuatia maneno ya msemaji wa wizara ya mambo ya nje wa Marekani kuhusu kiongozi wa Libya Moammar Gadaffi.

Shirika hilo la taifa la mafuta lilisema jana Alhamisi kuwa limewapigia simu maafisa wa kampuni ya mafuta ya Marekani na kuwaambia kuwa maneno kama hayo yanaweza kuharibu uhusiano wa kibiashara kati ya Marekani na Libya.

Libya inataka iombwe radhi na Marekani kufuatia maneno ya utani yaliotolewa na msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya Marekani P.J Crowley.

XS
SM
MD
LG