Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Machi 28, 2024 Local time: 21:34

Miaka 4 ya Kikwete: Watanzania wanasema nini?


Wakati Rais Jakaya Mrisho Kikwete wa Tanzania anatimiza miaka minne madarakani wananchi wa Tanzania wamekuwa na maoni mbali mbali kuhusu utendaji kazi wa kiongozi huyo ambaye anakabiliwa na uchaguzi mwingine mwakani.

Katika kipindi hicho cha miaka minne serikali yake imekuwa ikishutumiwa vikali na wananchi pamoja na vyama vya upinzani katika suala la ufisadi. Lakini baadhi ya wananchi na wachambuzi wanaona pia kuwa kiongozi huyo alipata mafanikio katika sehemu mbali mbali za maendeleo ya nchi.

Tanzania inatarajiwa kufanya uchaguzi mkuu wa Rais na wabunge mwaka ujao. Sauti ya Amerika imezungumza na Profesa Xavery Lwaitama wa chuo kikuu cha Dar Es Salaam, pamoja na wananchi wa kawaida ambao wanatoa maoni yao.

XS
SM
MD
LG