Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Aprili 18, 2024 Local time: 13:44

Kenya yataka Somalia isaidiwe kuleta uthabiti


Rais Mwai Kibaki wa Kenya amewasihi viongozi wa eneo la Maziwa Makuu kusaidia kuleta uthabiti nchini Somalia. Akiongea mbele ya wakuu wa nchi na viongozi wengine wa juu kwenye mkutano wa siku moja wa kimataifa kuhusu Maziwa Makuu, Bwana Kibaki aliwataka washiriki kuchukua jukumu la juu kuhakikisha kuna Serikali ya Kidemokrasia nchini Somalia. Bwana Kibaki alizungumzia uharamia kwenye pwani ya Somalia, akisema una athari mbaya kwa eneo na biashara ya kimataifa na pia kwa mazingira.

XS
SM
MD
LG