Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 11:15

Odinga Alihutubia Bunge


Waziri Mkuu Odiga alilihutubia bunge kwa mara ya kwanza kama waziri mkuu baada ya mabadiliko ya utaratibu wa bunge ambapo waziri mkuu atakuwa akipewa nafasi ya dakika 45 kila wiki kuhutubia bunge kuhusu masuala muhimu ya kitaifa.

Kabla ya mabadiliko hayo yaliyofuatia kuundwa kwa serikali ya mseto nchini Kenya, ni rais peke yake aliyekuwa akiruhusiwa kutoa hotuba maalum kuhusu sera na mipango ya serikali kwa ujumla.

Miongoni mwa masuala yaliyochukua uzito katika hotuba ya Bwana odinga ni kuhusu madai kuwa yeye na ndugu yake walihusika na tatizo la upungufu wa chakula nchini humo ambapo watu wasiopungua milioni 10 walikabiliwa na tatizo la njaa.


Zinazohusiana

XS
SM
MD
LG