Pakistan imetangaza siku moja ya maombolezo, nayo Lebanon imetangaza siku tatu za maombolezo, huku serikali kadhaa zikitoa salamu za rambirambi kwa Iran baada ya kifo cha Rais Ebrahim Raisi na waziri wa mambo ya nje Hossein Amirabdollahian katika ajali ya helikopta.