Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Mei 18, 2024 Local time: 14:29

Wanawake waandamana DRC kutaka vita vikomeshwe


Watu wakikimbia mapiagano kati ya jeshi la serikali na kundi la waasi la M23 Februari 7, 2024.
Watu wakikimbia mapiagano kati ya jeshi la serikali na kundi la waasi la M23 Februari 7, 2024.

Mamia ya wanawake wa Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo waliandamana siku ya Jumatano mjini Kinshasa wakitaka vita kukomeshwa huko mashariki mwa nchi yao ambako mapigano yamezidi katika siku za hivi karibuni kati ya wanajeshi wa serikali na waasi wa M23.

Wakiongozwa na waziri wa masuala ya jinsia, familia na watoto nchini humo, Gisele Ndaya, waandamanji hao walimebeba mabango yalionadikiwa matamshi mbali mbali kutaka mvita vimalizike,

Miongoni mwa waandamanaji hao ni pamoja na wanasiasa wanawake, na watumishi wa umma wakitoa shinikizo la kusitishwa kwa vita Mashariki mwa DRC na wakidai haki kwa takriban wahangaa millioni mbili walitokana na vita vita hivyo iliyoanza tangu mwaka 1994.

Wanawake hao waliva mavazi ya rangi nyeusi wakiandamana hadi katika Jengo la Ikulu ya rais, ambako waziri Gisele Ndaya aliwasilisha rasmi hati ya kushutumu kuhusika kwa Rwanda katika nchi yao na kupora mali asili ya DRC.

Mwishoni mwa wiki iliyopita, vijana waliandamana katika mji mkuu wa Kinshasa wakitaka mataifa ya Magharibi na Umoja wa Mataifa kuondoka DRC wakiwashutumu kwa unyonyaji wa malia sili ya taifa hilo na kuwezesha mapigano kuendelea.

Forum

XS
SM
MD
LG