Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumanne, Aprili 22, 2025 Local time: 12:27

Ulaya bado yakabiliwa na kiwango kikubwa cha mfumuko wa bei


Benki kuu ya Ulaya, Alhamisi imesema kwamba mfumuko wa bei bado uko juu, na kutangaza kama ilivyo tabiriwa kuongezeka kwa mara ya saba mfululizo katika viwango vyake vya riba muhimu toka Julai mwaka jana ambapo ilikuwa ni asilimia 0.25 ambayo ilikuwa ndogo mpaka hivi sasa.

Akiongea na wanahabari mjini Frankfurt, Ujerumani, Rais wa ECB, Christine Lagarde amesema wakati kiwango cha mfumuko wa bei kimeshuka kutoka kile cha juu cha zaidi ya asilimia 10 mwezi Oktoba, bado asilimia 7 inabaki kuwa cha juu sana.

Benki hiyo imesema viwango vilivyopita vyote ambavyo vilikuwa kati ya moja na nusu mpaka robo tatu ya poiniti ya asilimia, kinasambazwa kote katika sekta ya fedha ya muungano wao.

Bado haijawa wazi hata hivyo namna kinavyoweza kuathiri ya kiuhalisia kwa uchumi.

XS
SM
MD
LG