Samanta Power ambaye ni mkuu wa USAID, ambalo ni shirika kuu la misaada ya kimataifa la serekali ya Marekani, amesema kwamba wameamua kufanya uamuzi mgumu wa kusimamisha msaada wa chakula wa USAID mkoani Tigray mpaka watakapo toa taarifa zaidi.
Shirika hilo hivi karibuni lilianzisha msaada mwingine wa chakula uliokuwa na dhamirra ya kupelekwa kwa watu wa Tigray ambao wanakabiliwa na hali ya ukame lakini ulihamishwa na kuuzwa kwenye masoko ya kawaida amesema Samantha Power katika taarifa yake.
WFP pia imesema imesimamisha usambazaji wa chakula mkoani Tigray baada kutambua tatizo la vyakula kupelekwa kwenye kusiko stahili.