Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Februari 10, 2025 Local time: 02:58

Bondia wa Uingereza Anthony Yarde apata wasi wasi  dhidi ya bingwa wa wa uzani wa light-heavyweight Artur Beterbiev


Artur Beterbiev na Anthony Yarde walipokutana ana kwa ana wakati wa kupima uzito huko Brent Civic Centre, London, Uingereza Januari 27, 2023. Reuters
Artur Beterbiev na Anthony Yarde walipokutana ana kwa ana wakati wa kupima uzito huko Brent Civic Centre, London, Uingereza Januari 27, 2023. Reuters

Bondia wa Uingereza Anthony Yarde alisema anapata wasi wasi  kabla ya kukabiliana na bingwa wa kutisha wa uzani wa light-heavyweight Artur Beterbiev huko London siku ya Jumamosi.

Beterbiev mzaliwa wa Russia ameshinda kila pambano kati ya mapambano yake yote 18 kwa njia ya KO na ndiye bingwa pekee wa dunia mwenye uwiano wa ushindi wa asilimia 100 kwa njia hiyo ya KO.

Bondia huyo mwenye umri wa miaka 38 atapigana tena kupitia bendera ya Canada kama alivyofanya aliponyakua taji la WBO kutoka kwa Joe Smith Jr. kwenye ukumbi wa Madison Square Garden huko New York ambako alishinda kwa KO katika raundi ya pili Juni mwaka jana.

Mshindi huyo wa taji la WBC, WBO na IBF kutoka Dagestan aliwakilisha Russia wakati wa michuano ya olimpiki akiwa bondia wa ndondii za ridhaa aliyeng’aa katika michuano ya ridhaa na katika Michezo ya Olimpiki ya London mwaka 2012, lakini sasa anaishi Montreal na ana pasipoti ya Canada.

XS
SM
MD
LG