Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Aprili 19, 2024 Local time: 10:17

Brazil: Pele aendelea kukumbukwa na wananchi huko Sau Paulo


Brazil: Pele aendelea kukumbukwa na wananchi huko Sau Paulo
please wait

No media source currently available

0:00 0:01:27 0:00

Pele, mchezaji mashuhuri wa soka wa Brazil aliyeondoka kwenye umaskini wa kutembea peku peku hadi kuwa mmoja wa wanasoka wakubwa na wanaojulikana sana katika historia, alifariki dunia Alhamisi akiwa na umri wa miaka 82.

Pele, mchezaji mashuhuri wa soka wa Brazil aliyeondoka kwenye umaskini wa kutembea bila ya viatu hadi kuwa mmoja wa wanasoka wakubwa na mashuhuri wanaojulikana sana katika historia. Kifo cha mwanasoka huyo pekee aliyeshinda Kombe la Dunia mara tatu akiwa mchezaji kilithibitishwa na binti yake Kely Nascimento kwenye Instagram. Mchezaji huyo wa hali ya juu alikuwa akitibiwa saratani ya utumbo mpana tangu 2021. Alikuwa amelazwa hospitali mwezi uliopita akiwa na maradhi mengi. Aliibeba Brazil hadi kwenye kilele cha soka na kuwa balozi wa kimataifa wa mchezo huo katika safari iliyoanzia mitaa ya jimbo la Sao Paulo, ambapo alicheza mpira wa kutengenezwa na soksi iliyojaa magazeti au matambara.

XS
SM
MD
LG