Zaidi ya muongo mmoja tangu mapinduzi maarufu nchini Tunisia yaliyomuondoa madarakani dikteta Zine El Abidine Ben Ali vyama vya upinzani vimehimiza kususia uchaguzi huo ambao wanasema ni sehemu ya mapinduzi dhidi ya demokrasia pekee iliyojitokeza kutokana na vuguvugu la mapinduzi ya kiarabu ya 2011