Shambulio hilo baya limetokea saa chache kabla ya Israel kuapisha bunge lake jipya, huku wabunge wenye msimamo mkali wa mrengo wa kulia wakiwa tayari kuwa mawaziri, wakiapa kuwa watapambana na ghasia za Wapalestina.
Jeshi la Israel limeripoti shambulio la kisu karibu na eneo la viwanda la Ariel, kaskazini mwa Ukingo wa magharibi.
Taarifa ya jeshi la Israel imesema “Gaidi alifika kwenye mlango wa kuingilia eneo hilo na kuwachoma kisu raia katika eneo hilo.”