Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Desemba 04, 2023 Local time: 16:24

Milio ya risasi imesikika Jumamosi siku moja baada ya mapinduzi Burkina Faso


Mji wa Ouagadougou nchini Burkina Faso. September 30, 2022
Mji wa Ouagadougou nchini Burkina Faso. September 30, 2022

Milio ya risasi ilisikika katika mji mkuu wa Burkina Faso siku ya Jumamosi na wanejshi weyenye silaha nzito walipita katikati katika msafara, siku moja baada ya Rais Paul-Henri Damiba kuondolewa madarakani katika mapinduzi ya pili ambayo nchi hiyo ya Afrika Magharibi imeshuhudia mwaka huu.

Haikufahamika mara moja kilichokuwa kikiendelea na hakuna taarifa zozote kutoka kwa kiongozi mpya Kapteni Ibrahim Traore, ambaye aliwekwa na kundi lile lile la maafisa wa jeshi ambao walimsaidia Damiba kutwaa madaraka katika mapinduzi ya Januari 24.

Siku ya Ijumaa, Traore alionekana kwenye televisheni ya taifa, baada ya siku moja iliyokumbwa na milio ya risasi karibu na kambi ya jeshi, mlipuko karibu na ikulu ya rais na televisheni ya taifa ilizima matangazo.

Akiwa amezungukwa na wanajeshi, alitangaza serikali kuvunjwa na mipaka kufungwa. Haijulikani mahali alipo Damiba.

Utulivu ulirejea tena mjini Ouagadougou mapema Jumamosi lakini sauti ya risasi zilisikika majira ya mchana na kuonekana kwa msafara wa wanajeshi maalum kulisababisha maduka kufungwa na baadhi ya watu kukimbia kwa ajili ya usalama wao.

XS
SM
MD
LG