Uganda imesheherekea miaka 60 ya Uhuru wake Jumapili huko katika viwanja vya Kololo jijini Kampala.Rais Yoweri Museveni katika hotuba yake alitoa wito wa ushirikiano wa kibiashara kwa mataifa ya Afrika Mashariki na kuacha utegemezi wa kuagiza bidhaa kutoka nje ya kanda hiyo.