Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Aprili 26, 2024 Local time: 04:20

Mwanahabari wa kimarekani mwenye asili ya India akataliwa kuingia nchini humo


New Delhi Television (NDTV) microphone is seen on roadside in New Delhi
New Delhi Television (NDTV) microphone is seen on roadside in New Delhi

Mwanahabari wa kimarekani mwenye asili ya India ambaye pia hutengeneza makala za televisheni, amekataliwa kuingia India akiwa na familia yake baada ya kuwasili uwanja wa ndege wa New Delhi wiki iliyopita

Angad Singh ambaye hutengeneza makala za televisheni za kituo cha Vice News, aliwasili India kwa ajili ya kuwasalimia ndugu na jamaa, akiwemo mama pamoja na bibi na babu yake wakati alipokataliwa kuingia India na maafisa wa idara ya uhamiaji katika uwanja wa ndege mama yake alisema.

Angad aliwasili katika uwanja wa kimataifa wa Gandhi akitokea Marekani majira ya saa mbili na nusu usiku siku ya Jumatano, alimueleza mama yake Gurmeet Kaur kwa njia ya ujumbe wa simu.

Mwanahabari huyo ambaye ana uraia wa Marekani ameitembelea India mara kadhaa na amewahi kutengeneza makala siku za nyuma kuhusiasa na masuala ya maandamano ya wakulima, janga la Covid-19, na maandamano ya waislamu wa Kashmir.

XS
SM
MD
LG