Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Aprili 20, 2024 Local time: 07:37

Mwenyekiti wa tume ya Umoja wa Afrika alaani mashambulizi ya anga ya Israel


Mousa Faki Mwenyekiti wa tume ya Umoja wa Afrika Moussa Faki Mahamat.
Mousa Faki Mwenyekiti wa tume ya Umoja wa Afrika Moussa Faki Mahamat.

Mwenyekiti wa tume ya Umoja wa Afrika siku ya Jumapili alilaani mashambulizi ya anga ya Israel huko Ukanda wa Gaza huku ghasia zikiongezeka katika eneo hilo lenye machafuko, huku Wapalestina 31 wakiripotiwa kuuawa.

Moussa Faki Mahamat analaani vikali mashambulizi ya anga yanayoendelea kufanywa na Israel huko Gaza ambayo yamesababisha vifo vya zaidi ya raia 30 wa Palestina, wakiwemo watoto 6, taarifa ya AU ilisema.

Kuwalenga raia na kuendelea na ukaliaji wa kimabavu unaofanywa na vikosi vya usalama vya Israel ni ukiukaji mkubwa wa sheria za kimataifa, na kuleta shida katika utafutaji wa suluhu ya haki na ya kudumu”, ilisema taarifa hiyo.

XS
SM
MD
LG