Waziri Mkuu wa Sri Lanka alikubali kujiuzulu Jumamosi baada ya viongozi wa chama katika bunge kumtaka yeye na rais kuondoka madarakani katika siku ambayo waandamanaji walivamia makazi na afisi ya rais kuelezea hasira yao juu ya mzozo mbaya wa kiuchumi unaloikumba nchi hiyo.