Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Februari 15, 2025 Local time: 07:25

Chama tawala Nigeria chapata mwenyekiti mpya


Mwenyekiti mpya wa chama cha APC, nchini Nigeria Seneta Abdullahi Adamu akizunguma na wafuasi wake baada ya kuteuliwa Jumaomosi usiku.
Mwenyekiti mpya wa chama cha APC, nchini Nigeria Seneta Abdullahi Adamu akizunguma na wafuasi wake baada ya kuteuliwa Jumaomosi usiku.

Chama tawala nchini Nigeria kimemteua mwenyekiti mpya katika kongamano la kitaifa linalonuia kumaliza mizozo huku kikijiandaa kumchagua mgombea atakayechukua nafasi ya Rais Muhammadu Buhari katika uchaguzi wa mwaka 2023.

Buhari, ambaye alichaguliwa kwa mara ya kwanza mwaka wa 2015, alitumia wiki kadhaa kujadiliana na magavana wa majimbo na wajumbe wa chama ili kushinikiza msimamo wa makubaliano kabla ya kongamano siku ya Jumamosi.

Jumamosi usiku chama kilikubali Abdullahi Adamu, seneta ambaye alikuwa akiungwa mkono na Buhari ili kuepusha mizozo zaidi, kulingana na kamati ya uchaguzi ya chama cha All Progressives Congress (APC).

Ushindani wa kisiasa tayari umeanza kuchukua nafasi ya Buhari kama kiongozi wa taifa hilo lenye watu wengi zaidi barani Afrika lakini kinyang'anyiro hicho kimesalia wazi huku vigogo kadhaa wakichuana.

XS
SM
MD
LG