Rais wa Ghana Nana-Akufo Addo na mawaziri wake wamepunguza mishahara yao kwa kiwango cha asilimia 30 kama hatua za kupunguza matumizi ya serikali, wakati nchi inakabiliwa na gharama kubwa za mafuta kutokana na mzozo wa Ukraine na kukwama kwa mswada wa sheria kuhusu kodi mpya.