Baraza la Amani na Usalama la Umoja huo limeandika kwenye ujumbe wa Twitter kwamba wajumbe wake 15 wamepiga kura kusitisha Burkina Faso kushiriki kwenye shughuli zote za AU hadi pale utawala wa kikatiba unarudishwa nchini humo.
Jumuia ya uchumi ya nchi za Afrika Magharibi ECOWAS tayari ilishasitisha uwanachama wa Ougadougou tangu Ijuma na kupeleka ujumbe wakijeshi siku ya jumamosi kukutana na baraza tawala la kijeshi (MPSR).
Hii leo, Ujumbe wa mawaziri wa mambo ya nje wa nchi za jumuia hiyo unatarajiwa katika mji mkuu wa Ougadougou, ambako utakuwa na mazungumzo pia na viongozi wa baraza hilo la kijeshi.