Rais wa Ufilipino Rodrigo Duterte ametangaza kwamba atagombea nafasi katika baraza la senate katika uchaguzi mkuu mwaka ujao.
Tangazo hilo lililotolewa na msaidizi wake, linamaliza uvumi uliokuwepo kwamba Duterte alikuwa anapanga kushindana na binti wake katika kugombea nafasi ya makamu wa rais
Vyama vya kisiasa nchini Ufilipino vinakamilisha kuandaa orodha ya wagombe akatika nafasi mbalimbali kuelekea uchaguzi mkuu, siku ya mwishi ikiwa ni leo jumatatu.
Duterte haruhusiwi kugombea urais kwa mara nyingine, lakini anaweza kugombea nafasi nyingine.
Binti yake, Sara, amejiandikisha pia kugombania nafasi ya kiti cha makamu rais.
Uchaguzi utafanyika mwaka ujao 2022.