Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Januari 19, 2025 Local time: 05:39

Hesabu ya kura inaendelea Afrika kusini


Maafisa wa tume ya uchaguzi Afrika kusini wakihesabu kura
Maafisa wa tume ya uchaguzi Afrika kusini wakihesabu kura

Hesabu ya kura inaendelea nchini Afrika kusini katika uchaguzi wa madiwani wa serikali za mitaa.

Uchaguzi huo umetajwa kuwa mtihani kwa umaarufu wa chama kinachotawala cha African national congress ANC.

Chama hicho kilipata asilimia 54 ya kura katika uchaguzi wa manispaa wa mwaka 2016.

Maafisa wa tume ya uchaguzi wanasema hawataraji wapigaji kura wengi kujitokeza kwani hata walojiandikisha walikua wachache.

Matokeo rasmi yanatarajiwa kutolewa baadaye wiki hii.

XS
SM
MD
LG