Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Aprili 18, 2024 Local time: 13:29

CNARED inamtaka Mkapa kuahirisha mazungumzo ya Arusha kuhusu Burundi


Mkutano wa viongozi wa CNARED mjini Brussels
Mkutano wa viongozi wa CNARED mjini Brussels

Muungano wa vyama 25 vya upinzani vya Burundi CNARED, unamtaka mpatanishi wa mzozo wa Burundi, rais wa zamani wa Tanzania Benjamin Mkapa kuahirisha duru ya nne ya mazungumzo ya Arusha ili kuruhusu pande zote kushiriki.

Pancrace Cimpye msemaji wa CNARED Burundi.
Pancrace Cimpye msemaji wa CNARED Burundi.

Akizungumza na Sauti ya Amerika kutoka Brussels siku ya Jumanne baada ya muungano huo kuwachagua viongozi wake wapya msemaji wake Pancrace Cimpaye, anasema hadhani duru hii ya mazungumzo itaweza kuleta suluhisho la kweli.

please wait

No media source currently available

0:00 0:05:01 0:00

Anasema tatizo kubwa ni kwamba "baada ya matayarisho ya muda mrefu muungano mkubwa wa upinzani CNARED haujaalikwa na kwamba serikali pia haijapeleka wajumbe basi ni makubaliano gani yatafikiwa hapo Disemba 8 kama ilivyopangwa?"

Kiongozi mpya wa muungano huo unaojulikana kama Baraza la Kitaifa kwa ajili ya Kuheshimu Makubaliano ya Arusha ni Dk. Jean Minani aliyekua spika wa bunge la Burundi mara mbili, mara ya mwisho ikiwa kati ya 2002 hadi 2005.

XS
SM
MD
LG