Misri imethibitisha kwamba imemkamata mzalishaji wa kituo cha televisheni cha Al-jazeera, kituo cha utangazaji ambacho kwa kiasi kinafadhiliwa na familia inayotawala ya Qatar, kwa kwa habari za uchochezi kwa niaba ya taasisi hiyo ya habari.
Wizara ya mambo ya ndani imemtaja mtu huyo kuwa ni Mahmoud Hussain, ambaye alikamatwa Ijumaa kwa shutuma za kuvuruga usalama na kusambaza taarifa za uongo. Al-Jazeera ilisema Misri ilimkamata Hussain kwa mashtaka ya kutunga, baada ya kusafiri nchini humo kwenda kuitembelea familia yake na inataka aachiliwe huru mara moja.
Tukio hili ni la karibuni katika mfululizo wa ukamataji waandishi wa habari wa al-Jazeera nchini Misri, ikiongeza wasi wasi mkubwa juu ya uhuru wa waandishi wa habari wanaofanya kazi nchini humo.