Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Aprili 19, 2024 Local time: 02:30

Wakuu wa kanisa watapendekeza suluhisho kwa mzozo wa DRC


Askofu Luis Mariano Montemayor, wapili kutoka kushoto mwakilishi wa Vatican huko DRC akitembea na maskofu wenzake kuelekea ukumbi wa mazungumzo Kinshasa. Dismeba 8 2016 (VOA/Top Congo)
Askofu Luis Mariano Montemayor, wapili kutoka kushoto mwakilishi wa Vatican huko DRC akitembea na maskofu wenzake kuelekea ukumbi wa mazungumzo Kinshasa. Dismeba 8 2016 (VOA/Top Congo)

Baraza la Kitaifa la Viongozi wa Kidini la Jamhuri ya Kidemokrasia ya kongo CENCO, linalosimamia upatanishi kati ya serikali na upinzani, litawasilisha Alhamisi pendekezo la kutanzua mzozo wa kisaisa nchini humo.

Georges Kapiamba, mwakilishi wa asasi za kiraia akiwa moja wapo wa wajumbe 16 wa tume ya majadiliano kati ya serikali na upinzani ameiambia Sauti ya Amerika kwamba, Maaskofu wa Kanisa la Katholiki, wanadhani wana pendekezo la kutanzua mzozo uliyopo.

Hadi hivi sasa tofauti kuu iliyopo ni juu ya mamlaka ya Rais Joseph Kabila wakati wa kipindi cha mpito, baada ya muda wake rasmi kumalizika hapo Disemba 19.

Vyama vikuu vya upinzani vilivyoungana chini ya jina jipya la Rasemblement walosusia mazungumzo yaliyoongozwa na Umoja wa Afrika, wanataka serikali ya mpito ikiwa itaongozwa na Kabila au la ni lazima ipunguze sana madaraka ya kiongozi huyo.

Halikadhalika upinzani unataka uchaguzi ufanyike mnamo mwaka ujao wa 2017, huku serikali na baadhi ya vyama vya upinzani vinataka uchaguzi ufanyike 2018.

Bw Kapiamba, akiwa katika tume maalum ya majadiliano anasema ana matumaini kwamba pande zote zitaweza kufikia makubaliano kabla ya sikukuu ya Krismasi kama vile Maskofu wanavyotaka.

Bank Ki-moon atoa wito

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon, akisalimiana na Rais Joseph Kabila Kabange, wa Kongo na Rais Paul Kagame wa Rwandakwenye makao makuu ya UM, Sept. 27,
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon, akisalimiana na Rais Joseph Kabila Kabange, wa Kongo na Rais Paul Kagame wa Rwandakwenye makao makuu ya UM, Sept. 27,

Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon, ametoa wito Jumatano jioni kwa wadau wote huko Kongo, kuhakikisha wanafikia makubaliano katika mazungumzo yanayoongozwa na viongozi wa kidini.

Katika taarifa yake Bw. Ban amesisitiza kwamba "kupunguza mvutano na kubuni mazingira yanayostahiki ya kufanikiwa majadiliano yanayosimamiwa na Cenco katika muda mfupi uwezekanavyo ni muhimu, pamoja na kutayarisha uchaguzi wa kuaminika na wazi".

Polisi wakipiga doria kutawanya maandamano
Polisi wakipiga doria kutawanya maandamano

Katibu Mkuu alilaani pia vifo vilivyotokea Jumatatu na jumanne wakazti wa ghasia baada ya muda wa muhula wa pili wa Kabila kumalizika. Maandamano katika miji mbali mbali ya kongo yalikandamizwa na polisi na kiusababisha vifo vya karibu watu 19

XS
SM
MD
LG